Waziri wa elimu Profesa George Magoha atangaza mtihani wa darasa la nane na kidato cha nne kufanya mwezi wa April 2021 iwapo shule zitafunguliwa mwezi wa Septemba.Waziri aliyazungumza haya akiwa mjini Nakuru.
Waziri alisisitiza kuwa mipango yote ya maandalizi ya shule kufunguliwa yanafanyiwa kazi na wizara ya elimu na washika dau wote ikiwepo wizara ya afya.Miongoni mwa miundo msingi inayofanyiwa kazi ni;
- Ukaguzi wa shule zote kuhakikisha zinapata maji na uwezekaji wa matangi ya maji.
- Idadi yote yawanafunzi pamoja na shule kujulikana ili kujumuishwa katika mikakati ya ufadhili wa vifaa dhidi ya COVID 19.
- Utengezaji wa maski zitakazo tosheleza idadi ya wanafunzi wa shule na msingi pamoja na sekondari.
- Uagizaji wa viyeyuzi iwapo baadhi ya shule zitakosa maji ya kutosha.
- Walimu kupimwa virusi vya CORONA kabla kufunguliwa kwa shule mwezi September 2020.
- Walimu kupata mafunzo kwakina maambukizi na usambaaji wa Ugonjwa wa Virusi vya CORONA
- Kutengwa pesa Zaidi za kuongeza madarasa shule za msingi na sekondari.
- Kutenga pesa za madawati ya kutosha kufikia lengo la wanafunzi kukaa umbali wa mita moja.
Shule zitafunguliwa iwapo kamati mbali mbali za kutathmini uwezekano wa shule kufunguliwa na kuzingatia usalama wa wanafunzi shuleni wataafikiana.Juhudi zote zote za kuhakikisha shule zitafunguliwa zinaendelea .Waziri alitamatisha kwa kusema kuwa shule zitafunguliwa tu endapo hali ya usambaaji na maambukizi ya ugonjwa COVID 19 utadhibitiwa.